Posts

Showing posts from January, 2021

Je Umetokea Kumpenda mtu aliye na Mpenzi wake na Hujui nini cha Kufanya ?? Soma Hapa Upate Majibu

Image
Mapenzi yamekuwa yakichukua nafasi kubwa sana  katika maisha yetu ya kila siku na yamekuwa yakichangia kwa kiasi kikubwa furaha kwa kila mtu.  Kama huamini, angalia wale waliotokea kupenda na wao wakapendwa, utabaini nyuso  zao zimetawaliwa na furaha isiyo na kifani. Lakini mapenzi hayo hayo yamekuwa ni chanzo cha  vilio kwa baadhi ya watu.  Mpenzi msomaji wangu, kupenda hakuna macho! Moyo ukishapenda hausikii la kuambiwa. Katika hili ndiyo maana unaweza kumuona mwanaume kazimika kwa demu ambaye hawaendani kabisa lakini moyo wake ndiyo umeshapenda.  Ilishawahi kutokea msichana akampenda kijana mmoja ambaye ni fukara kupita maelezo. Yeye akawa ndiyo anamhudumia kwa kila kitu. Akamfanyia mpango wa ajira na mwisho wake wakafunga ndoa.  Sasa hivi wanaishi maisha ya furaha na amani. Wamegeuka mfano wa kuigwa kwa jinsi wanavyopendana lakini huko nyuma msichana huyo alikuwa akichekwa kwa kutoa penzi kwa mwanaume asiye na mbele wala nyuma.  Hayo ndiyo map...

Kama wewe ni Mwanaume Muoaji basi Jiandae na Mambo Yafuatayo.

Image
KUNA kelele nyingi sana kutoka kwa akina mama, wakilia kutendwa na wenza wao. Nimewahi kukutana nao wengi sana, wakilalamika na ukijaribu tu kuwagusia kuhusu nia yako ya kutaka urafiki nao, utawasikia: “Weee, tena sitaki hata kumsikia mtu anaitwa mwanaume.” Na unapotaka kujua kulikoni, atakupa simulizi ndefu juu ya uhusiano wake wa kimapenzi ulivyokatishwa ghafla na mwenza wake kutokana na sababu mbalimbali, lakini kubwa huwa ni kukosa uaminifu.  Ninataka kuwapa siri, siyo tu wanawake, bali hata wanaume.Wakati mwingine tunajiumiza mioyo yetu sisi wenyewe, kwa sababu tunatumia muda mwingi kujipa mawazo ambayo yanatuondolea furaha tunayopaswa kuwa nayo kwa muda mwingi. Kufikiri sana kuhusu mwenza wako ni ugonjwa ambao mwenye uwezo wa kuutibu siyo mwingine zaidi yako. Na ugonjwa huo unatokana na kosa ambalo wewe ulilifanya siku ile ya kwanza ulipoamua kuanzisha uhusiano wa kimapenzi naye. Kuna wanawake wanasema wanaume ni waongo sana, kwamba watakudanganya kwa maneno matamu, lakini wa...

KWA WADADA: MBINU ZA KUMTEKA MUMEO ASICHEPUKE HIZI HAPA

Image
  WANAWAKEhwengi wengi wanashindwa kujua wao wanatofautiana na wanaume kwa hisia na hata mawazo ya mapenzi. Wanaume wana mambo wanayoyapenda kutoka kwa wake zao hasa katika masuala ya mapenzi. Kwanza wanawake wajue wanaume  wana hisia za haraka za kufanya mapenzi kuliko wanawake. Mwanaume alivyoumbwa ni kwamba akiona tu mfano mwanamke umevaa kanga moja au umevaa night dress hiyo inatosha kusisimua. Wapo wanawake wanaowasisimua waume zao bila wao kujua. Mfano umevaa tu kanga moja au night dress ndani huna kitu. Kwako ni jambo la kawaida lakini kwa mwanaume sio la kawaida kwa kukuona hivyo tayari unakuwa umeamsha hisia zake. Ukimwona anakuja kutaka haki yake usidhani anakusumbua. Ujue tayari mwenzako alishafiria mbali zamani we huna habari. Ni vyema ukawa mwangalifu kujua hisia za mwanaume huyo mumeo kama inawezekana mpe anachohitaji kwani usipofanya hivyo unamwathiri kisaikolojia na anaweza kufikiria nje. Wanawake wengi wa nje waliowaweka waume zenu kiganjani hiyo ndio mbinu wa...

DALILI ZA MWANAUME KUPUNGUZA MAPENZI KWA MWANAMKE

Image
  DALILI YA 1 Mwanaume anaanza kuonyesha hasira na kuhamaki kwenye kila unachokifanya hata kama ni kitu kidogo. Hii ni kwasababu penzi limempungua au kumuisha na hivyo anakosa uvumilivu kwako. Anaweza kukupayukia hata ukiwa katikati ya watu na wala hatojali unavyo jisikia kwa yeye kufanya hivyo. Utashangaa na kujiuliza mbona huko mwanzoni aliweza kunivumilia? Jibu ni kwamba penzi limepoa au kuisha – Chris Mauki DALILI YA 2. Kwa kawaida mwanaume anavyompenda mwanamke huwa na kiu ya kumfurahisha,  hufanya vitu kuhakikisha mpenzi wake anatabasamu na anajisikia murua. Kilasiku kiu ya mwanaume ni kuona mwanamke huyo anatamani kuendelea kuwa ndani ya penzi hilo. Mapenzi yakiisha vitu hivi vyote vinayoyoma na kupeperukia mbali – Chris Mauki DALILI YA 3. Mapenzi ya mwanaume yanapokwisha kwa mpenzi wake anakosa kabisa kuwa na muda naye. Mwanzoni mlikuwa mnakuwa na muda wa pamoja sasa hapati tena muda huo na kila ukiuliza unapewa visingizio kibao, mara kazi, mara ubize, mara safari, mar...

MAMBO SABA YANAYOWAUMIZA SANA WANAUME

Image
Kupitia safu yetu ya mahusiano, leo nimekuletea makala maalum hasa kwa wanawake kutokana na malalamiko ya wanawake wengi kuwapoteza waume zao. Kilio chao kikubwa ni kukimbiwa na wanaume au kuachwa. Leo anakuwa na mwanaume huyu, baada ya muda mfupi kunatokea chokochoko, mwanaume anatimka zake. Jamaa anamkimbia na kwenda kuanzisha uhusiano mwingine. Baada ya kukimbiwa, mwanamke hakati tamaa. Anaanzisha uhusiano mwingine, ndani ya muda mfupi tu, anaambulia maumivu tena. Anabaki kujilaumu. Hajui chanzo cha yeye kukimbiwa. Matokeo ya hili, mwanamke anapoteza uelekeo. Kila mwanaume anayekutana naye anamkimbia. Mwisho wa siku anajikuta umri umeenda. Kuolewa inakuwa ni ndoto. Anaanza kulazimisha kusaka mtoto ili angalau na yeye aitwe mama. Wanaume wengi hujikuta wakiwaacha wapenzi wao kwa sababu ya tabia fulani ambazo wakati mwingine huanza taratibu na baadaye huwa kikwazo kikubwa. Ili kuweza kuepukana na tatizo hili ni vyema tukaangalia vitu ambavyo wanaume wamekuwa hawavipendi kutoka kwa wan...

MBINU ZA KUPATA MTAJI WA BIASHARA

Image
  WATU WENGI WANATAMANI KUMILIKI BIASHARA SIKU MOJA NA HUENDA WANA MIPANGO MIZURI JUU YA BISHARA ZAO. MIPANGO HII INAWEZA IKAWA VICHWANI TU AU MINGINE KATIKA MAADISHI LAKINI INAPOFIKA WAKATI WA UTEKELEZAJI WA MIPANGO HII UKOSEFU WA MTAJI WA BIASHARA HIYO NI KIPINGAMIZI KWA WENGI. LAKINI KUNA JINSI KADHAA AMBAZO ZINAWEZA KUSAIDIA UPATIKANAJI WA MITAJI KWAJILI YA BIASHARA.  AINA ZA MITAJI KUNA AINA MBILI YA MITAJI KWAAJILI YA BIASHARA AU UWEKEZAJI WA AINA YOYOTE. MTAJI WA MKOPO MTAJI WA MMILIKI  MTAJI WA MKOPO UNAKUWEZESHA KUKOPA TOKA KWA TAASISI ZA FEDHA AU MTU BINAFSI WAKIWEMO NDUGU ,JAMAA NA MARAFIKI NA KUHITAJIKA KULIPA KATIKA KIPINDI MAALUMU IKIWA PAMOJA NA RIBA AU BILA RIBA. AINA HII YA MTAJI INAKUWEZESHA KUFANYA BIASHARA LAKINI NI LAZIMA UWE MAKINI KATIKA UTUNZAJI WA FEDHA ZAKO NA UZALISHAJI WAKE KWANI MWISHOWE UTAHITAJIKA KURUDISHA FEDHA ZOTE PAMOJA NA RIBA PENGINE KILA MWEZI.  MTAJI WA MMILIKI NI MTAJI TOKA KWA MTU AU KAMPUNI AMBAYO INAHITAJI KUWA NA UMILIKI W...