Posts

Showing posts from June, 2021

Sababu 5 kwanini kila mahusiano mapya unaishia kuachwa!

Image
Unajiona kama mtu mwenye laana, kila ukiingia kwenye mahusiano hayakai muda mrefu, mahusiano yako yanakaa miezi miwili au hata hiyo haifiki unaachwa.unajihisi kuchanganyikiwa, unajiona mbaya, unahisi huwezi kupendwa basi hizi zinaweza kuwa ndiyo sababu unaachwa na si hizo zilizopo kichwani kwako. (1) Unaenda kwa kasi sana kila unapoanzisha mahusiano. Umekutana na mtu, hata hamjajuamna vizuri ushamuambia kila kitu chako, ushaanza kumtambulisha kwa marafiki zako kama mke/mume, ushaanza kutaka kujua kwao, kutaka mfanye vitu pamoja, kuongelea habari za mtoto, unaonyesha mchecheto wa hali ya juu. Kwa mwanaume ukiwa hivi wanawake wenaweza kukupapatikia na kuona uko siriasi ila ukizidisha sana mwanamke mwenye akilia tajiuliza kwanini una haraka, labda kuna kitu unakificha hivyo kurudi nyuma. Kwa mwanamke ukiwa hivi mwanaume anakuona kama umechanganyikiwa sana kuhusu ndoa, anakuona huna maisha na utamsumbua hivyo kukuacha kwani anahisi utakua mzigo kwake. (2) Unalalamika sana kuhusu ma...

MAMBO 5 YA KUZINGATIA KAMA UNAUNGANISHWA NA MWANAUME USIYEMJUA

Image
! Inaweza kuwa ni Kanisani labda huyo mwanaume kapirtia kwa mchungaji kuwa anakutaka wewe, ni msikitini, labda kuna shehe kamfuata Baba yako kuwa kuna mtu kakupenda. Inaweza kuwa ni shoga yako, Mama yako, au dada yako, mtu unayemheshimu anakuja na kukuambia kuwa kuna Kaka anakupenda na anataka kukuoa. Ndoa ni jambo jema ila kabla ya kuona na mwanaume ambaye humjui zingatia mambo haya. (1) Achana na stori za kusikitisha kuhusu huyo Mwanaume na chunguza kwanza; Wengi ya wanaume wanaounganishwa wanakuja na stori nzuri, mara huyu Kaka kaumizwa sana, mara huyu kaka alikua na mwanamke kamuacha na watoto, mara anataka kuoa, ni mstaarabu, umekutanishwa kanisani unasikia ni mchamungu, Shehe anakuja anakuambia ni muumini mzuri, basi dada yangu kabla ua kukubali chunguza. Acha kuamini kila kitu unachoambiwa hata kama umeambiwa na mchungaji au shehe, umeambiwa na mtu unayemuamini, dada yako au shoga yako. Kuna baadhi ya wanaume huficha tabia zao kwa kutafuta wtau unaowaheshimu ili uwaamini...

Kuna mahusiano makubwa kati ya mtoto na baba wakati akiwa tumboni, au mtoto na mtu ambaye mama yake anampenda.

Image
Wanaume wengi sana huwadharau wanawake wanapokuwa mjamzito, Hawajui kipindi cha ujauzito ndio kipidi cha kuchota moyo halisi wa mwanamke. Kwa lolote unalomfanyia wakati wa ujauzito kwa mwanamke analiweka moyoni, na hatowahi kulisahau maana ndio kipindi cha kujua nani na yupi anayempenda na kumthamini wakati wote. Jinsi mwanaume atakavyokuwa akiishi kwa furaha na upendo wakati wa ujauzito wa mpenzi wake, Ndivyo mtoto anavyorithi furaha ya wazazi akiwa bado tumboni. Maana wataalam na watu wa imani husema kuwa mtoto anasikia akiwa tumboni, na wanasayansi hukazia kuwa hisia za mama yake ndizo zinazompa uhakika wa namna hatari au furaha... *WABABA,* *WAKAKA,* *WANAUME NA VIJANA WA KIUME* *TUNAPOIHUSUDU NGONO TUWE TAYARI KWA MATOKEO YATOKANAYO NA VITENGO HIVYO.* Follow my page Share

KANUNI 6 MUHIMU KWA AJILI YA MAHUSIANO YAKO

Image
  * 1:MFAHAMU VIZURI MTU UNAYEHUSIANA NAYE;* Awe ni mke au mme wako, hakikisha unamfahamu vizuri Na kama hamjaoana, muda wa mahusiano hadi uchumba ndio muda mzuri wa kufahamiana kuelekea kwenye ndoa. Hakikisha unamfahamu katika maeneo yake tofauti tofauti, Je Yeye ni mtu wa aina gani (haiba gani) ? Anapenda nini ? Kitu gani hapendi ? Hali yake ya mahusiano na Mungu ikoje ? Je uchumi wake uko vipi ? Je marafiki zake ni wapi ? Je unazifahamu ndoto zake za maisha ? Je anapenda miziki gani ? Je ndugu zake wa karibu ni wapi ? Je anaabudu wapi na nani anamlea ? Je anapendelea mlo gani sana ? Je anapenda kusoma kitabu gani haswa ? Je unazo ndoto zipi hapo mbeleni ? Na je umechukua hatua gani kuwa mtu huyo unayetaka kuwa ? Je unataka maisha yako yawe vipi baada ya miaka 5 ijayo ? Ni nani anakuhamisisha na unataka kuwa kama yeye ? Ukiweza kuyafahamu hayo na mengine mengi itakusaidia uweze kuishi naye Vizuri na kusaidiana vizuri. Kumfahamu vizuri mwenzi wako husaidia kupunguza migogoro min...

HII NI MIONGONI MWA KAULI ZA KIJINGA NA KIPEPO KUSEMA KUWA MWANAMKE HANA DINI

Image
* Huu ni moja ya msemo wa wanadamu unaotumika hasa kwa mwanamke anapotakiwa kuolewa na mtu wa imani tofauti na yeye. Wanaposema mwanamke hana dini wanakuwa wanamaanisha kwamba mwanamke hana haki au uhuru wa kuwa na msimamo wake binafsi wa kiimani. Basi watu huwa wanamshauri binti wakisema, wewe olewa tu bwana mwanamke hana dini yeye popote tu anaenda. Wakiwa wanamaanisha kwamba kile anachokiamini mume atakayemuoa ndicho atakachokiamini na yeye. Yaani kama yeye anamuamini au anamuabudu Mungu aliye hai na anayetaka kumuoa anaabudu mti, basi aachane na Mungu aliye hai afuatane na mume wake waanze kuabudu mti. Mwanamke, huu msemo si kweli kwamba wewe hupaswi kuwa na msimamo wako wa kiimani au wa kuabudu. Wanawake na wanaume sote tutasimama mbele ya kiti cha hukumu, siyo kwamba watakaohukumiwa ni wanaume peke yao. Ukiruhusu ndoa ikakutoa kwenye imani yako na kukupeleka kwingine hiyo ni juu yako, Mume wako, ndoa yako wala watu waliokushauri olewa tu hawatakusaidia usiende Jehanum. Binti usiw...

JE HUA UNAJIPODOA PINDI ANAPORUDI MUMEO AU NDOO MPAKA UTOKE NA MASHOGA ZAKO!

Image
Dada yangu, mama yangu je una tabia ya kujiandaa kwa ajili ya mumeo??? kwa maana hua unavaa nguo za kumvutia na kupaka ka simple makeup kwa ajili yake?. Mapenzi ni ubunifu na asikudanganye mtu usipochacharika na mumeo watakuchakarikia wanaoweza kazi hio. Asikuambie mtu mwanaume anapenda kumkuta mkewe kajiandaa kwa ajili yake, anapenda kukuta mkewe kabadilisha style ya mavazi yake au nywele zake Sio kila siku twende kilioni utadhani yale mananasi ya mwisho wa msimu Siku moja moja ingia YouTube angalia namna ya kubana nywele, namna ya kufunga lemba zuri kwa ajili ya kumvutia mumeo. Kaa ukijua usipomvutia wewe watamvutia wengine. Najua mtasema wanaume hawaridhiki ila ushawahi kujaribu kumtuliza na hakutulia? au ndo fata mkumbo tu? Maana nawaona sana mnasema ohoo wanaume hawaridhiki, sasa tutalidhika vipi na mambo unafanya Mara moja kwa mwaka??? wee pendeza uone navyo kupeleka mbuga za wanyama ukawaone kidogo Na hata kama haridhiki mfanye akitoka ajute, maana hana anachokikosa kwa mkewe up...