Posts

Showing posts from April, 2021

KAMA NDIYO UMEMALIZA CHUO BASI JUA KUA HAKUNA MILIONI 10 ZINAKUSUBIRI MTAANI!

Image
Kama ndiyo umemaliza chuo unatakiwa kujua kua hakuna milioni kumi ambazo zinazurura mtaani na kukusubiri wewe ili uzifanyie biashara. Unatakiwa kujua kua hakuna mzazi ambaye atahangaika kukulipia ada, atakopa na kujinyimka ili usome halafu urudi umuambie nipe na milioni kumi nikafanya biashara na kama wapo ni wachache sana! Kwa wazazi wengi kusoma inaamanisha kuajiriwa na kama utamaliza chuo bila ajira inamaanisha umeshindwa maisha, kwa maana hiyo kama kijana ni lazima ujiongeze wewe mwenyewe, ni lazima uache kusubiri milioni kumi ndiyo ufanye biashara ya kisomi na kuabdilisha hiyo elfu kumi au laki moja ambayo ni rahisi kwako kuipata na kuifanya kuwa milioni kumi. Kama huwezi hivyo basi miaka mitano baadaye utakua umekaa sehemu unalalamika kua ajira hamna na utakutana na watu wengi wa darasa la saba ambao wana biashara zao na ukiwauliza walianza na mitaji kiasi gani watakuambia elfu kumi mpaka laki moja ambayo kwa wakati huo utakua huna au unayo lakini umri nao utakua umeenda....

ACHA KUMLAZIMISHA AHISI UNACHEPUKA ACHA KUFICHA KAMA HUNA CHA KUFICHA!

Image
MTEJA; Kaka mimi mume wangu ananisumbua anataka kushika simu yangu wakati mimi si shiki yakwake. Nimeweka password ila anakasirika yaani sijui hata nimfanye nini huyu mwanaume. IDDI MAKENGO; Kwanin kuna ubaya gani mume wako kushika simu yako, si mume, unaficha nini mpaka hutaki ashike, unachepuka? MTEJA; Hapana lakini kaka si ulisema kuwa kila mtu anatakiwa kuhangaika na simu yake na si mambo ya kuchunguliana kwenye simu. IDDI MAKENGO; Hapana, hukunielewa vizuri, nilisema hivii “Kama huna ubavu wa kumuacha mpenzi wako usiguse simu yake!” mume wako kuamua kushika simu yako inamaana yeye anajua kabisa kama akikuta madudu hataishia kulia na kuomba msamaha yeye anaweza kukurudisha kwenu na maisha yakaendelea. MTEJA; Lakini kaka mbona kama unawatetea wanaume kushika simu za watu. IDDI MAKENGO; Hapana dada, hata wewe unaweza kushika simu yake. Lakini utakayoyakuta huko basi unamaamuzi umuache au unyamaze na kisirani chako, lakini sio ushike, ukute madudu halafu umuambie aombe msamaha...

BOSI WANGU ANANITAKA KIMAPENZI NIFANYE NINI NA MIMI NINA MCHUMBA?

Image
Habari Kaka mimi ni binti wa miaka 27, sijaolewa ila niko wkenye mahusiano na mpenzi wangu huu ni mwaka wa nne. Ninafanya kazi katika kampuni moja ya ujenzi, sasa hapa kazini kuna Bosi wangu ambaye ni mmoja wa wamiliki wa hii kampuni, wapo wanne ila huyo ninayemzunguimzia ndiyo anasimamia sana. Sasahuyu Baba ni ananitongoza, ananisumbua kiasi kwamba anaweza kunipigia simu mpaka usiku, sasa boyfrienda wangu anakasirika na kudhani labda nipo kwenye mahusiano naye. mimi siko kwenye mahusiano naye kwani ni mtu wa wanawake, anatembea na karibu kila mwanamke anayefanya kazi, namjua na ninamkwepa. Lakini shida Kaka ni hivi, naona kama nisipomkubalia nitapoteza kazi yangu kwani huwa ana kawaida ya kuwafanyia figisu mpaka kufukuzwa kazi. Kwenye mahusiano yangu mchumba wangu naye haeleweki, kila nikimuambia suala la ndoa ananiambia kuwa nisubiri kwani bado anajipanga, sasa Kaka nahofia kama naweza kumkataa Bosi nikilinda penzi ila mwisho wa siku bado nikaachwa, naomba unisaidie nifanye n...

WATOTO WACHUO AMBAO MNADHANI MNAYAJUA MAPENZI KULIKO SISI WAKONGWE!

Image
Watoto wa chuo naomba niwaambie hivi, tunajua mnafanya mapenzi kweli lakini acheni kujiozesha. Hao wanafunzi wenzenu mnaotembea nao na kudanganyana kuhusu ndoa hawajajua kutafuta pesa, siku wakiingia mtaani maisha yakwapiga watasahau hata majina yenu. Kwa maana hiyo hembu wakiwaambia kuhusu kuzaa, sijui nakupenda, nipo tayari kufa kwaajili yako, wakikuambia ujinga kama beba mimba nikimaliza natafuta kazi waambieni kwaheri maana kazi hazipatikani kirahisi namna hiyo. Lakini nyie mnaotembea na waume za watu aisee hawawaachi wake zao. Mnaweza kujiona kama keki sasa hivi mkafikiri wake zao ni wajinga, hawajui mapenzi, hawajui kumhandle mume ila si kweli. Mnadanganywa, mkibeba mimba zao wanarudi kwa wake zao, kuna toafuti kati ya kununua bia na kununua Pampas. Kuna wale ambao mko kwenye mahusiano na vijana hawajaoa wana kazi zao mtaani. Nyie ndiyo mnaona ndoa hizi, wadogi zangu, watuw ana watu wao lakini hata kama hawana hembu punguzeni kudhani kama mnayajua mapenzi sana, mkabeba na...

MAMBO 5 YA KUWAAMBIA WANAWAKE WENYE KIPATO PALE TU WANAPOINGIA KWENYE NDOA

Image
(1) Hamuwezi majukumu ya kuhudumia familia hivyo msijaribu; Mwanamke hata awe analipwa milioni mia kwa siku lakini hawezi kubeba majukumu ya mwanaume kama vile kulisha familia, kulipa kodi, kusomesha watoto na vitu kama hivyo, atafanya kwa muda ila atachoka na kulalamika. Mwanamke anatakiwa kuchangia, hata kama anatoa kikubwa lakini anapaswa kuchangia kwakua wanawake wanachoka, akihudumia familia kidogo tu anahisi kama kabebeshwa mzigo wa mawe hivyo kuichoka ndoa mapema, kwa maana hiyo ukiingia kwenye ndoa tu, muachie mume wako majukumu yake kwani yatakushinda tu. (2) Muache mume wako awe mwanaume mwanzo tu wa ndoa; Muache mume wako awe mwanaume, yeye ndiyo aamue kuwa mtaishi wapi kwa maana kulipa kodi au la, aamue watoto watasoma wapi na apange mambo yote. Hata kama umemzidi kipato lakini ni wajibu wake yeye kama mume kupanga hayo mambo, mwanzo kabisa wa ndoa usiwe na hataka ya mafanikio na kulazimisha mambo ambayo mume wako hana uwezo nayo. (4) Msaidie mume wako kwa kuongezea...

🌺SIFA ZA BINTI ANAETAKIWA KUOLEWA🌺.

Image
Madame Dorcus nimekuandalia somo.🙄🙄 🌺👉Mwenye upendo wa dhati na sio tamaa 🌺👉Msafi na kwenye kutunza mazingira ya nyumbani 🌺👉Mkarimu anayependa kuwasiliana ana ushirikiano mzuri na wenzake wazazi na jamii inayomzunguka 🌺👉Usiwafukuzie mwanaume acha waone thaman yako yako hapo itakuwa umejijengea msingi lakini ukijichekesha kwao si jambo zuri. 🌺👉Wanaume wanathamini kile walichokihangaikia kwa tabu,lakini vya kupata kiurahisi wap huvishusha thamani jitunze,jiamini,jikubali na jipende wewe kama binti. 👉Mcha Mungu(Maana ndoa inachangamoto nyingi inahitaji Dua na maombi ya kutosha kuombea ndoa na familia)🤲👏 🌺👉Mwenye maonyo na mfanikishaji wa mipango sio umepata mchumba kila sàa unapiga simu  🔹naomba ya salon 🔹nataka kwenda out, 🔹mama yangu anaumwa 🔹nataka kwenda kwa shangazi wiki ijayo Binti huyu si mfanikishaji wa mipango Anayejua kupika,anayependa kujifunza hata kama hajui kupika.

UNADHANI NI MWANAMKE YUPI AMBAYE ANATESEKA ZAIDI HAPA

Image
ZAHARA; Ameolewa, mume wake anamhudumia kwa kila kitu lakini hatakia toke, saa kumi na mbili anatakiwa kurudi nyumbani. Kutoka ni mpaka ruhusa ya mume, hajaruhusiwa kufanya kazi amefunguliwa tu Biashara hapo nyumbani. Haruhusiwai kupost picha zake kwenye mitandoa ya kijamii, mume anashika simu yake na kuhoji kila kitu. JACKLINE; Ameolewa, mume wake anamhudumia kwa kila kitu, ameruhusiwa kurfanya kazi, anaweza kutoka wakati wowote, anaweza kurudi nyumbani saa tisa usiku mume hata hamuulizi ulikua wapi. anaweza kutoka na marafiki wakiume lakini mume hamuulizi. Anaweza kuaga anaenda kwenye shetehe Zanzibar akakaa wiki mbili mume hata haulizi uko wapi, mume hashiki simu yake, anaenda kwao kila akitaka anaweza kulala nnje na mume asiulize, anamuachia mume wa toto na mume hajali. Niambie, katim ya hao waiwili unadhani ni yupo angalau ana furaha na ni kwanini?

MAMBO YA KUEPUKA UWAPO CHUMBANI

Image
🌹 *DONDOO ZA NDOA*🌹 EPOSODE YA 4 ✍️ Leo Dr.Charles nimekuandalia mambo ya kuepuka unapokuwa na mwenzako chumbani...Hii ni episode ya 4 1.Epuka kwenda kulala mda (wakati) tofauti na mmeo. Mme kalala chumban wewe upo sebulen au wewe unaanza kulala kabla ya mmeo.. Hapa najua kuna watu hawatakubali kabisa😃 ila ukweli ndio huo..  2.kuwa bize na simu au tv ukiwa kitandan hii utafsiliwa kama dharau yaan umemdharau mmeo👌 3.kupanda kitandani ukiwa mchafu ujaoga😂 au hujajisafisha uke,ujanyoa mavuz, hii umfanya Mme akinai kufany mapenz na wewe... 4.kulala kitandani na Mme huku unahasira hii utafsiriwa kuwa unakiburi na umemchoka Mme👌 5.kuwa bubu chumbani upo na mmeo kitandani upo kimya mda wote, upo serious km upo na kaka yako👉hii umfanya Mme hakose hamu ya kukuanza ✍️ 6.kutoa visingizio Mme akionyesha kutaka mzigo 👉hii ndio hatar kbs hupelekea Mme kuchepuka,   _TIBU Chanzo_

🌹MAMBO AMBAYO YATAMFANYA MUMEO/MPENZI WAKO AKUCHOKE 🌹

Image
KARIBU KATIKA SOMO LETU. ✍️✍️ *----•<°○●🍃🍇🍃●○°>•----* 🍃🍇Uzuri wa mwanamke unapatikana kwenye ulimi wake.Tuache tabia ya jeuri na maneno machafu,kiburi na dharau hakika tabia hizi zinamchukiza kila mwenye akili. *🍃🍇KAZI KWANZA* Baadhi yetu tunathamini na kujali kazi zetu na hatuna muda na mahusiano yetu. *🍃🍇WATOTO KWANZA MUME BAADAE* (KWA WANANDOA) Kuna baadhi yetu tukishakupata watoto mapenzi yote yanaelekea kwa watoto na tunamsahau baba watoto. *🍃🍇KUTOKUA NA SHUKRANI* Hii ni tabia sana itayomchokesha mumeo na aondoshe mapenzi kwako, kua na shukrani kwa yale anakufanyia ndipo atakapopata moyo wa kukufanyia makubwa zaidi. *🍃🍇KUTOKUA MUELEWA* Kuna baadhi yetu tunakua ving'ang'anizi na tukitaka kufanya letu hata tukakatazwa hatuskii wala hatujali kua tumeolewa tuwe wenye kutii waume zetu. *🍃🍇USIRI* Tuko baadhi yetu tunakua tunawaficha waume zetu kila kitu hatuwafanyi wao kua ndio washauri wetu. *🍃🍇KUKOSOA KILA JAMBO* Tuache tabia ya kukosoa na kugomb...

Fahamu mambo unayotakiwa kuyaepuka wakati Wa kwenda kulala na mmeo

Image
KARIBU KATIKA SOMO✍️✍️✍️✍️ Madame Dorcus nmekuandalia somo hili👇👇 ❤💋💋❤💋❤💋❤ *fahamu mambo unayotakiwa kuyaepuka wakati Wa kwenda kulala na mmeo* 🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥 👉kama mke unatakiwa kuepuka tabia hizi pindi uingiapo chumbn kulala na mmeo ❤kwenda kulala mda (wakati) tofauti na mmeo 👉Mme kalala chumban wewe upo sebulen au wewe unaanza kulala kabla ya mmeo ❤kuwa bize na simu au tv ukiwa kitandan 👉hii utafsiliwa kama dharau yaan umemdharau mmeo👌 ❤kupanda kitandani ukiwa mchafu 👉ujaoga au hujajisafisha uke,ujanyoa mavuz, hii umfanya Mme akinai kufany mapenz na wewe ❤kulala kitandani na Mme huku unahasira 👉hii utafsiriwa kuwa unakiburi na umemchoka Mme👌 ❤kuwa bubu chumbani 👉upo na mmeo kitandani upo kimya mda wote, upo serious km upo na kaka yako👉hii umfanya Mme hakose hamu ya kukuanza  ❤kutoa visingizio Mme akionyesha kutaka mzigo 👉hii ndio hatar kbs hupelekea Mme kuchepuka,  mmeo apagawe kwako.

💞💞FAHAMU KUHUSU MWANAMKE✍️✍️💞💞

Image
💞💞💞Madame _DORCUS_ nimekuandalia somo hili wewe mwanaume yamkini unaishi na mkeo/mpenzi wako  ila inatakiwa ufahamu kuwa👇👇👇💞💞 ,💞💞Mwanamke ni kiume wa aina yake na Mungu katika kumuumba alimpa akili ya pekee sana, ndio maana hata vitabu vya dini vinasema uishi nae kwa akili.😅😅😅💞💞 💞💞💞Nasema akili kwa kuwa mwanamke hajapewa nguvu kama   ww maana ww unaweza mpiga ila yeye akatumia akili yake na ukabaki unashangaa tu.💞💞 💞💞Familia nyingi zilizofahanikiwa nyuma yake kuna mwanamke, kama unapingana hilo fatilia utapata majibu mazuri. Au hujawahi ona mtu anamtesa mkewe halafu anamfukuza maisha yake yanabadilika ghafla ww ubadhani ni kwa nn? Amka usingizini💞💞 💞💞Mwanamke akikupenda anaweza fanya chochote kwa ajili yako au anaweza ishi na ww bila kujali unamaisha ya aina gani, unaweza ukakuta hadi marafiki au watu wanamshangaa kufikria kakupendea nn? Ila ndio upendo huo.🤐💞💞 💞💞Na hata kama utamtesa au utamtukana ataendelea kukukpenda tu maana...

UKIWASIKILIZA WATU HAWA SANA UNAWEZA KUCHANGANYIKIWA KUHUSU NDOA!

Image
Moja ya sababu kubwa ya wanawake kuteseka kwakua tu hawajaingia kwenye ndoa ni ndugu. Kuna presha kubwa ya ndugu, majirani na sehmeu za ibada kwa mwanamke hasa anapofikisha miaka 30 bila ndoa. Wengi huona kama ndiyo maisha yake yameisha kwamba anahitaji kuwa na mwanaume ndiyo awe na furaha. Ndugu humtenga, marafiki humtenga na hata katika nyumba za ibada kuna vitu vingi hatakiwi kushiriki kwakua tu hajaolewa. Hii huwapelekea wanawake wengi kuingia kwenye ndoa za mateso bila kufikiria mara mbili ili tu kuridhisha jamii na wao kuonekana wameolewa. Kama uko katika hali hii unapaswa kujua mambo makuu mawili. Jambo la kwanza nikuwa, ndoa hupangwa na Mungu hata hao wanaokupigia kelele kuwa utaolewa lini hawakujipangia ndoa na siku zote wakati wa Mungu ndiyo wakati sahihi. Hivyo hivyo kwa mtoto, hupangwa na Mungu na wala mtoto haletwi na ndoa au kelele za ndugu zako. Jambo la pili ni hivi, ukiachana na wazazi wako ambao tangu siku ya kwanza ya maishaa yako wao hukutakia mema wengine w...

MWANAUME ACHA KULAUMU, HEBU MFANYIE MKEO AU MPENZIO HAYA UONE TOFAUTI

Image
1. Mpe muda wako. Usimfanye aombe muda wako. Tengeneza muda kwa ajili yake. Tengeneza wakati ambao mtakuwa mkifurahi na kupiga story pamoja. Usiwe bize Jumatatu mpaka Jumapili. Wanawake hupenda sana kusikilizwa na waume zao. 2. Msifie pale anavyofanya jitihada ya kuwa na muonekano mzuri. Pale anaposuka mitindo mipya ya nywele, anavyovaa nguo nzuri na hata anapokupikia chakula kitamu. Mwanamke husikiliza mno maoni ya mwanaume ampendae. Mu-appreciate mke wako, nae atafanya kila kitu kwa ajili yako. 3. Wanaume ni wazito kusema "samahani". Yani kuna wanaume anajua kabisa kakosea lakini anaona akimwambia mkewe au mpenzi wake samahani ni kama amedhalilika au amedharaulika. Sikiliza, iko hivi hili neno samahani wala halikupunguzii uanaume wako. Kuomba msamaha sio UDHAIFU, mashujaa na watu wenye nguvu na hekima ndio wanajua siri na nguvu iliyopo ndani ya neno samahani. Pale unapomkosea muombe Msamaha. Hii itaonesha ni kwa kiasi gani unathamini moyo wake.  4. Mnunulie zawadi, ...

MWANAUME AKISHAKUACHA KUBALI KUACHIKA HAPASWI KUWA RAFIKI YAKO!

Image
Najua mpo wengi, najua mnaumia, najua mnachanganyikiwa, lakini kama mwanaume akikuacha na kwenda kuoa mwanamke mwingine hapaswi hata kuwa rafiki yako. Narudia, kama ulikua kwenye mahusiano na mwanaume, si mahusiano yale ya tia maji tia maji, hapana! Mahusiano yale mnapendana mpaka kila mtu anajua kuwa yeye ndiyo mume wako, lakini ghafla bila sababu akakuacha na kwenda kuoa mwanamke mwingine. Bado unampenda lakini kakuacha, hujamkosea kitu lakini kakuacha, alikua anakuaminisha kuwa wewe ndiyo mke lakini kakuacha. Basi dada yangu huyo mwanaume kata mawasiliano naye, narudia, kata mawasiliano naye. Hapaswi kuwa rafiki yako achilia mbali kuendelea kuwa mpenzi wako. Najua unampenda sana lakini mwanaume kama huyo atakurudisha nyuma na utaishia maumivu tu. Kwanza hawezi kumuacha mke wake kwaajili yako, pili hata akimuacha mke wake hatakuoa wewe kwani hakukuhitaji tangu mwanzo, tatu anakuharibia kwa wanaume wengine. Kila mwanaume akija na kutaka kukuoa anawmabiwa una mtu wako kumbe ni ...

ACHA KUWA MWANAMKE WA KULALAMIKA TU, TAMBUA JUHUDI ZA MUME WAKO

Image
Moja ya sababu kubwa za wanaume wengi kuchelewa kuoa ni kujiandaa kiuchumi kwaajili ya kutengeneza familia.  Mwanaume amelelewa na kukuzwa katika jamii ambayo inaamini kua katika familia ni jukumu lake kuhudumia famila yake kiuchumi na kuhakikihsa mke na watoto wake wanakuwa na maisha mazuri. Hii ndiyo maana kijana hukakikisha kuwa anakua na uwezo wa kuhudumia familia kabla ya kuoa. Tofauti na mwanamke ambaye anaweza kuolewa hata bila kuwa na kazi na akaendelea kubaki kuwa Mama wa nyumbani katika maisha yake yote ya ndoa, mwanaume hawezi kufanya hivyo. Hata kama mkewe atakuwa na kila kitu, kwa maana ya pesa lakini bado mwanaume atahitaji kufanya kazi na kuchangia chochote ndani ya familia. Huo ndiyo uanaume, mwanaume kamili hujisikia vibaya pale anapokuwa ni mtu wakulishwa na mkewe au hata tu mkewe anapokosa mahitaji muhimu ambayo alipaswa kumpa. “Mwanamke unapolalamikia kitenge kipya, mchango wa haursi, Kitchen Party, saluni na vitu vingine hata kama si vya muhimu. Hata ka...

NINGEKUA MIMI WEWE NINGEKUA NA SUBIRA KWANI NDOA HAIJI KWA HARAKA KIHIVYO!

Image
Wanawake wengi, kila wanapofikisha miaka 25, wakitongozwa wanawaza ndoa. Najua, ndiyo, unakua ushamaliza chuo unatafuta kazi, au hukusoma sana hivyo uko mtaani muda mrefu, una maumivu ya nyuma umeshaumizwa kimtindo hivyo unataka mtu siriasi wa kukuoa. (1) Mwanaume anakuja, anakupa stori za hapa na pale na kukuambia anataka kukuoa; Ukweli nikuwa, haijalishi kakuambia nini, asilimia 95 ya mambo anayokuambia mwanaume kabla ya kukupata kimapenzi ni uongo ili tu akupate. (2) Ameshakuapata, hajakuacha, amekaa na wewe miezi miwili au mitatu unaanza kukumbushia kuhusu ahadi zake za nyuma kuwa atakuoa; Ukweli nikuwa, miezi miwili mpaka mitatu mwanaume bado hajaamua kama anakupenda au la, hajaamua kuwa wewe ni mtu sahihi au la. Tena mwingine inawezekana hata bado hajaachana vizuri na X wake. Ukipiga kelele katika miezi hii ya mwanzo ni ngumu sana kupata mwanaume kwakua, aliachana na X wake kwasababu ya kelele kama zako za unanioa lini, wakaanza kufanyiana vituko kisha anakuja kwako, hata...

MBINU TATU AMBAZO WANAUME HUTUMIA KUKUACHA KISTAARABU!

Image
Sidhani kama ni usataarbu lakini wanaume wengi huona kama ni njia rahisi ya kumuacha mwanamke ambaye wamekaa naye muda mrefu, mwanamke hajafanya kosa lolote na walishaahidi ndoa sasa wameshindwa kumuacha kwani mwanamke ni king’ang’anizi anavumilia kila kitu. Wanaume siku hizi wanatumia mbinu hizi tatu, kuna nyingine nyingi ila leo tuangalie gia hizi tatu; (1) Anakuomba Mapenzi kinyume na maumbile; Hii ni kubwa sana na ni kama kamtindo kwa wanaume wengi. Anataka kukuacha lakini hataki uje kumlaumu kuwa kakupotezea muda, akijua kuwa kama una akili utakataa anakuambia “Kuna kitu nilikua sijakuambia, mimi napenda kufanya mapenzi kinyume na maumbile siwezi kuishi bila hiyo kitu hivyo kama unataka tuoane basi nipe na kama huwezi basi bora kuachana maana nitakusumbua, bila hiyo kitu nitachepuka” Anategemea una akili, utakataa atakuacha, ila kama wewe ni Kizibo, utakubali atakufanyia hivyo na bado atakuacha. (2) Anakuomba umchukulie mkopo umpe pesa kubwa;Kuna wengine anataka kukuacha l...

Kabla ya kumvulia nguo mwanaume mme wa mtu ebu jiulize Mambo yafuatayo!

Image
➡️Kwanini hakukuoa wewe? Kama kweli ungekua Ni mtu wa thamani kwake na Kuna kitu anakiona kizuri kwako ambacho anajua kinamsaada mkubwa kwenye kujenga familia yake angekuoa lakini kwakua huna sifa na vigezo vya wewe kujenga familia pamoja ndio maana anaishia kukutamani tu na Kama anakwambia anakupenda fahamu kua anakudanganya. Anakutumia tu na baada ya siku hautakua nae kwa sababu Hana anachokipoteza kwako ➡️ Kama amepata ujasiri wa kukutamani wewe fahamu kua Kuna wengine wengi amewatamani na wewe siyo wa Kwanza, usidhani kua utakua wewe peke yako kwa sababu tayari Ni tabia ambayo anayo na kila atakapomwona mwingine atamtamani na kuanza mahusiano naye, kwahiyo uki expire atakuona wa kawaida Kama anavyowaona wengine wa kawaida akiwemo mke wake! Na hili kwa wanaume inabidi kubadilika na kulizika na mke wako, unachokitafuta nje hakipo kizuri zaidi ya mke wako, kipendezeshe Cha kwako,ukiwa na shauku ya kwenda lodge mwandae mke wako mtoke naye na ukitaka kwenda out toka naye, Mfurah...

TAZAMA NYUMA KWA KUJIFUNZA SI KWA KUJUTA

Image
Kila kitu kilichotokea katika maisha yako hakikutokea kwa bahati mbaya, kuna sababu ya kila kitu kutokea hata kama ni kibaya.  Chukulia changamoto ulizopitia katika maisha yako kama darasa  na kamwe usiangalie nyuma kwa kusononeka na kujilaumu. Acha kuumiza kichwa katika mambo ambayo sasa huwezi kuyabadilisha. Kumbuka ubaya wa jana nikuwa  imeshapita, haiko tena mikononi mwako na huwezi kuibadilisha, lakini kesho bado haijafika na unaweza kuitumia leo kutengeneza kesho yako nzuri kwa kujifunza kutoka jana.  Kuna mambo mengi ambayo yamepita ambayo kama ungepata nafasi ungeyafanya tofauti. Yachukulia mambo hayo kama darasa na anza kufanya tofauti sasa. Wewe kuwa hai leo ni nafasi ya kuyabadilisha mambo hayo na si kuendelea tu kujuta. Image result for happy black coupleAcha kuishughulisha akili yako katika kujuta, acha kupoteza muda wako katika majuto katika kuwaza laiti ningelifanya hivi aua vile, fanya sasa ambavyo ungetamani kufanya.  Kuna namna ambavyo ...

NINGEKUA MIMI WEWE NINGEKUA NA SUBIRA KWANI NDOA HAIJI KWA HARAKA KIHIVYO!

Image
Wanawake wengi, kila wanapofikisha miaka 25, wakitongozwa wanawaza ndoa. Najua, ndiyo, unakua ushamaliza chuo unatafuta kazi, au hukusoma sana hivyo uko mtaani muda mrefu, una maumivu ya nyuma umeshaumizwa kimtindo hivyo unataka mtu siriasi wa kukuoa. (1) Mwanaume anakuja, anakupa stori za hapa na pale na kukuambia anataka kukuoa; Ukweli nikuwa, haijalishi kakuambia nini, asilimia 95 ya mambo anayokuambia mwanaume kabla ya kukupata kimapenzi ni uongo ili tu akupate. (2) Ameshakuapata, hajakuacha, amekaa na wewe miezi miwili au mitatu unaanza kukumbushia kuhusu ahadi zake za nyuma kuwa atakuoa; Ukweli nikuwa, miezi miwili mpaka mitatu mwanaume bado hajaamua kama anakupenda au la, hajaamua kuwa wewe ni mtu sahihi au la. Tena mwingine inawezekana hata bado hajaachana vizuri na X wake. Ukipiga kelele katika miezi hii ya mwanzo ni ngumu sana kupata mwanaume kwakua, aliachana na X wake kwasababu ya kelele kama zako za unanioa lini, wakaanza kufanyiana vituko kisha anakuja kwako, hata...

MBINU TATU AMBAZO WANAUME HUTUMIA KUKUACHA KISTAARABU!

Image
Sidhani kama ni usataarbu lakini wanaume wengi huona kama ni njia rahisi ya kumuacha mwanamke ambaye wamekaa naye muda mrefu, mwanamke hajafanya kosa lolote na walishaahidi ndoa sasa wameshindwa kumuacha kwani mwanamke ni king’ang’anizi anavumilia kila kitu. Wanaume siku hizi wanatumia mbinu hizi tatu, kuna nyingine nyingi ila leo tuangalie gia hizi tatu; (1) Anakuomba Mapenzi kinyume na maumbile; Hii ni kubwa sana na ni kama kamtindo kwa wanaume wengi. Anataka kukuacha lakini hataki uje kumlaumu kuwa kakupotezea muda, akijua kuwa kama una akili utakataa anakuambia “Kuna kitu nilikua sijakuambia, mimi napenda kufanya mapenzi kinyume na maumbile siwezi kuishi bila hiyo kitu hivyo kama unataka tuoane basi nipe na kama huwezi basi bora kuachana maana nitakusumbua, bila hiyo kitu nitachepuka” Anategemea una akili, utakataa atakuacha, ila kama wewe ni Kizibo, utakubali atakufanyia hivyo na bado atakuacha. (2) Anakuomba umchukulie mkopo umpe pesa kubwa;Kuna wengine anataka kukuacha l...

MWANAUME AKISHAKUACHA KUBALI KUACHIKA HAPASWI KUWA RAFIKI YAKO!

Image
Najua mpo wengi, najua mnaumia, najua mnachanganyikiwa, lakini kama mwanaume akikuacha na kwenda kuoa mwanamke mwingine hapaswi hata kuwa rafiki yako. Narudia, kama ulikua kwenye mahusiano na mwanaume, si mahusiano yale ya tia maji tia maji, hapana! Mahusiano yale mnapendana mpaka kila mtu anajua kuwa yeye ndiyo mume wako, lakini ghafla bila sababu akakuacha na kwenda kuoa mwanamke mwingine. Bado unampenda lakini kakuacha, hujamkosea kitu lakini kakuacha, alikua anakuaminisha kuwa wewe ndiyo mke lakini kakuacha. Basi dada yangu huyo mwanaume kata mawasiliano naye, narudia, kata mawasiliano naye. Hapaswi kuwa rafiki yako achilia mbali kuendelea kuwa mpenzi wako. Najua unampenda sana lakini mwanaume kama huyo atakurudisha nyuma na utaishia maumivu tu. Kwanza hawezi kumuacha mke wake kwaajili yako, pili hata akimuacha mke wake hatakuoa wewe kwani hakukuhitaji tangu mwanzo, tatu anakuharibia kwa wanaume wengine. Kila mwanaume akija na kutaka kukuoa anawmabiwa una mtu wako kumbe ni ...

NAKOSEA WAPI MKE MWENZANGU HATAKI TUWE MARAFIKI?

Image
Mimi ni Mama wa watoto wawili, nimeolewa ndoa yangu ina miaka 7 sasa. Mimi na mume wangu tulikua vizuri sana, lakini mwaka juzi alioa mke mwingine. Kabla ya kuoa aliniambia, hatukua na tatizo lolote lakini aliniambia ni kwasabababu ya Dini. Ingawa niliumia sana lakini nilimkubalia na nikaonahakuna shida. Sababu ya kuja kwako Kaka ni hivi, huyo mke mdogo nashindwa kumuelewa. Alipoolewa nilimpigia simu kumkaribisha lakinia linijibu vibaya, nikawa nampigia simu kumsalimia lakini hataki salamu zangu, anaishia kunisonya, nikimuambia mume wangu mbona mke mwenzangu hataki tuongee hataki urafikia anasema nimuache tu atazoea. Kaka ni karibu mwaka wa tatu sasa nimeshaenda kwake mara moja ila hakunipoke vizuri, kwangu hajawahi kukanyaga na wala wanangu hataki kuwaona. Nashindwa kuelewa Kaka, niishije na mke mwenzangu, nikimueleza mume wangu ananiambia niachane naye, hivi Kaka watu mtaolewaje nyumba moja halafu muwe maadui?

HUHITAKI KUJITAMBULISHA KILA SIKU KUWA WEWE NDIYO MWANAUME, WANAJUA!

Image
Hakuna uanaume wowote katika kumpiga mke wako, hakuna kumfundisha kokote katika kumpiga. Uwezo wako wa kiakili ni mdogo kama unashindwa kukaa na mtu mzima ukaongea naye na mkaelewana. Haikufanyi kuwa na nguvu zaidi kama kila siku unampiga mke wako ambaye anakuheshimu na kukunyenyekea wakati ukifika ofisini unavumilia matusi na manyanyaso ya Bosi wako ambaye hata hana sababu ya kukutukana. Acha kujishaua kua una hasira za karibu kwa mkeo anaongea sana hivyo huwezi kujizuia, hapanab ni kitu ambacho unaamua kwakua unamuona ni mnyonge, kwakua hujiamini vyakutosha hivyo unadhani kuwa labda ukimpiga ndiyo atajua kuwa wewe ni mwanaume. Kama wewe kila siku ni kumuambia mkeo kuwa “Utanijua mimi ndiyo nani humu ndani?” Basi jua hata wewe hujijui ni nani? Simba dume hahitaji hata kunguruma ili kutambulika yeye ndiyo nani? Anajua kabisa yeye ni nani hivyo hahitaji kujitambulisha kila siku. Kama wewe ni mtu wa kujitambulisha kila siku basi jua kuwa kuna kasoro. Kama wewe unahitaji kumpiga m...

HII POST NI MAALUMU KWA VIJANA WA KIUME!

Image
Hivi kwanini baadhi yenu mmekuwa washenzi na wapuuzi kiasi hiki?? Umemfuatilia binti wa watu kwa zaidi ya miezi sita. Richa ya kukukataa na kukukwepa kwa kipindi chote hicho bado hukukata tamaa uliendelea kumfukuzia huku ukimuahidi furaha na mapenzi ya dhati Kwa roho nyepesi kama tunavojua wanawake wameumbiwa roho ya huruma binti wa watu akaamua kukubali ombi lako si kwa kukupenda bali kwakukuonea huruma na kwa kujali muda unaopoteza kwaajili yake. Ni kweli mwanzo hakukupenda lakini tangu alipokubali kuwa na ww taratibu akawa anakuweka moyoni mwisho wa siku akakupenda mazima. Kutokana na ahadi zako ukamfanya aweke imani yake kubwa kwako akitegemea siku moja utakuja kuwa mume wake. Sasa hata sijui uliitoa wapi hiyo roho ya kishetani Baada ya kumfunua funua na kumchezea mtoto wa watu kwa zaidi ya mwaka na miezi ukaamua kumtelekeza na kwenda kuanzisha mahusiano na mwanamke mwingine. Maskini binti wa watu kwa unyonge anakuuliza "Nimekukosea nini mpaka unifanyie hivo" Kwa ...

MAMBO AMBAYO MWANAUME ANAFANYA KUKUTEST KAMA MSICHANA UNAFAA KUWA MKE WAKE

Image
1. Ukienda kwake ukutane na vyombo vichafu na nguo chafu zimejazana usidhani ni mvivu, ni kamtihani anakupa. 2. Ukiingia kwake ukaona anampigia simu yule dada wa usafi anayekujaga mara moja kwa wiki aje afanye usafi alipwe usidhani eti anajali kihivyo. Anakutest aone kama utasema "Acha baby, ntakufulia mpenzi wangu". 3. Ukikuta kwake amefanya shopping ya vyakula vya kupika kama unga, mchele, na vingine halafu akakwambia mwende ule mgahawa fulani mkapate dinner usidhani eti ana hela kibao ya kutumia! Anakutest aone kama utamwambia mbaki kwake mpike mle. Uko chumba cha mtihani! 4. Siku kakuahidi kukutoa out halafu unafika kwake unakuta kajikunyata kama mgonjwa anakwambia mama ake kapiga simu anaumwa anaomba atumiwe hela. Halafu anakwambia hela aliyo nayo na ukipiga mahesabu unaona ni kama ile ya  kutumia mkiwa out. Anakuomba ushauri afanyaje. Wewe unamwambia "Baby twende out, suala la mama nina uhakika kaka zako na dada zako watalishughulikia, atawapigia". Woi...

KWA WANAUME TU..JUA MBINU 10 ZA KUFANYA ILI KUMFIKISHA MPENZI WAKO KILELENI HARAKA NA AKARIDHIKA.

Image
 kama huwezi kumfikisha mwanamke kileleni basi unausika katika hili somo!!!!...Wengi wakitaka kujua ni namna gani ya kumfikisha mwanamke kileleni kwa kuzani hawana nguvu za kuhimiri kufanya tendo kwa muda mrefu bila kufikiri kuwa kumuandaa mwanamke kabla ya tendo kunaweza kukusaidia katika kumridhisha. Wanaume wengi huwa hawana maandalizi mazuri kwa wanawake wao kabla ya tendo la ndoa yanayoweza kuwasaidia kama kichochezi cha kuwafikisha kileleni mapema. Basi njia hizi zinaweza kuwa msaada mkubwa endapo zitatumika ipasavyo na hata yule ambaye ulikuwa umridhishi baada ya somo hili utaweza kumlidhisha ipasavyo kwa kumfanyia yafuatayo. 1.Mpe maneno matamu okimtomasa kwa ulimi sikio lake kimahaba zaidi 2. Pitisha ulimi wako shingoni kifuani, tumboni, mapajani ni ikibidi zama chumvini walau kwa dakika kumi hivi 3. Tumia ulim wako ipasavyo kutomasa kitovu chake 4. Mnyonye lita kadhaa za mate na huku ukitumia ulimi wako ipasavyo kuuchanganya ulimi wake 5. Papasa matiti yake huku u...

ACHA KULAZIMISHA UPENDO KWA MCHUMBA WAKO AMBAE ANAONYESHA DALILI ZA KUTOKUTAKA TENA..

Image
Inafika mahali lazima tukubaliane na ukweli,upo na mahusiano na mchumba wako ila anakuonyesha dalili fulani za ovyo,vitendo vya kujeruhi moyo wako,usiendelee kubembelezana na mtu wa hivyo utajipa matatizo mengine...ambayo hata ukuwa nayo. Lazima tujue uchumba ni kivuli cha ndoa ikiwa mtu huyu ameanza kukuonyesha dalili za kukuchoka wewe ukafosi jua,hata ukiingia nae kwenye ndoa atakufanyia hayo na zaidi. Waswahili wanasema dalili ya mvua ni mawingu,sasa kama umeona izo dalili kaa pembeni uwenda Mungu nae anakuonya mapema ndo maana ameweka tabia zake wazi. Acha kuwa king'ang'anizi ukaingia kwenye ndoa na mtu wa namna hiyo,jua ni kujibebesha gunia la misumari. Raha uchumba ni kupenda wote isiwe mwingine ni mtumwa wa mwanzake,,ikiwa unaona ni ngumu kukaa pembeni muombe Mungu akuwezeshe maana kwa nguvu zako ni ngumu ....  Jiunge na group letu https://chat.whatsapp.com/CVHMF6BPooMGeJhz01l8VI

MAMBO 3 AMBAYO KILA MWANAMKE ANAPASWA KUYASAHAU ANAPOINGIA KWENYE MAHUSIANO MAPYA!

Image
(1) Umri wako; Hata kama una miaka 40, lakini katika zile hatua za mwanzo wa mahusiano, miezi sita ya kwanza, acha kabisa kuwaza kuhusu umri wako, kuwaza kama unazeeka, kuwaza kama kwa uymti huo hutapata mtu wa kukuoa. (2) Watu na Maisha yao; Kuna ndugu, kuna marafiki, kuna majirani na kila mtu anayekujua, wote wanataka uolewe, kuna kelele nyingi za kutaka uwe na mtotyo, uwe na mtu siriasi. Acha kuwawaza hao watu, furahia mahusiano yako na acha kuwaza wanakuonaje. (3) Kuhusu kuwa na mtoto; Labda kama unaona kuwa kalenda yako inaelekea kufika mwisho, labda ushafikisha miaka 38 mpaka 40 ndiyo suala la mtoto linapaswa kukuumiza kichwa. Tofauti na hapo, unapoingia kwenye mahusiano jiondolee ile presha ya kwamba nitapata mtoto kweli, nisipozaa, mbona haonekani kama Baba na vitu kama hivyo. Mambo haya matatu yanawasumbua sana wanawake. Wakiwaza kuhusu umri wkenda, nduguwa nanionaje na ile presha ya umti wangu unaenda bila mtoto wanakua na ptesha kubwa sana. kila wkaati unakua unawaza...

NI KITU KIDOGO LAKINI KINAFANYA NDOA YAKO IWE TAMU BALAA!

Image
Hata kama umezoeana vipi na mume wako, jifunze kumuomba mume wako ruhusa na si kumpa taarifa. Haijalishi umemzidi kipato wala unatoka kwenye familia ya kitajiri kuliko yeye. Haka kautaratibu kanakupunguzia maudhi mengi sana, kuna mambo mengi utaepuka kama ukijijengea haka ka utaratibu. Sio tu kama mume wako atahisi kuheshimiwa, lakini pia wewe itakufanya ujione mke. Mwanamke uhuru ukizidi sana anajiona mwanaume, anajiona kuwa anaweza kufanya chochote kile anachokiweza na kuna kashetani kanakuja kanakuambia umejaribu mume wako na hapo ndipo kila kitu kubadilika. Narudia, najua mnahisi kuwa haki sawa, mbona yeye aage mimi niombe ruhusa, lakini ukweli nikuwa, mwanamke mume wako akiwa ni wa kukuomba ruhusa si tu utamchoka bali utajisikia kama umeoa. Mbali na kuwa ni heshima kumuomba ruhusa ila kuna kale kakudeka flani ambako wanawake wakikataliwa kitu wanakua nako. Sio kwamba unapiga magoti au kuomba kama unaomba pumzi, lakini kama mmezoeana sana na mume wako hembu seba basi “Mume ...

KAMA UNA TABIA HII KILA UNAPOINGIA ONLINE JUA UNAHARIBUA MAHUSIANO YAKO!

Image
Kama ukiingia online, ukamuona mpenzi wako yuko online labda kwa nusu saa au masaa mawili bila kukutafuta unakasirika na kuhisi kuwa hakupendi, labda anachart na watu wengine, ukaona kama anakudharau basi jua kuwa una matatizo na unahitaji msaada, ni suala la muda tu utaharibu mahusiano yako. Iko hivi, katika mahusiano ni lazima umpe fursa mwenza wako kukumiss, kufanya vitu vingine zaidi yako. Kama ukiingia kwenye mitandao, hamna kitu cha kuchart ushatuma meseji, ‘hi’ huna stori halafu unataka yeye ndiyo alete stori basi jua kuwa unakosea, ana haki ya kuwa online na ana haki ya kutokujibu meseji zako kama hajisikii. Unapolazimishia kila dakika kuongea na wewe, kila dakika kuchart na wewe basi baada ya muda ataboroka. Hii ni kwa wote, wanawake na wanaume, yaani kama ni kuchart muwe na kitu cha kuchart, mwenzako naye apende na sio kwakua tu wewe huna kitu cha kufanya ulazimishie, na asipokua na mzuka wa kuchart unune, hiyo itakuharibia kila mahusiano. NB; Kama wote mnapenda ndiyo...

Mambo 5 yakufanya Unapojihisi/Unapogundua kuwa una tatizo la nguvu za kiume?

Image
  wa mwanaume hakuna kitu kigumu kama hiki, kuna ambao hugundua kuwa wana matatizo ya nguvu za kiume tangu wakiwa wadogo na kuamua kutokutafuta wanawake kabisa. Lakini kwa sasa kuna wengi ambao hugundua kuwa wana matatizo haya wakati wakiwa kwenye mahusiano au baada ya ndoa. Najua kama una hili tatizo ushahangaika sana na dawa, kuna wanaopona na ambao hawaponi, kuna ambao zinaisha kabisa na wengine huwa nazo kidogo. Najua ni ngumu kuishi na hili tatizo hivyo mbinu zifuatazo zitakusaidia sana kuishi kwa amani katika ndoa yako. 1. Sio mwisho wa ndoa yako wanawake wanaweza kukuvumilia Utaanza kwa kujidharau, kudhani labda mke wako atakuacha, kudhani labda atakudharau na kudhani labda ndiyo mwisho wa ndoa yako. Labda nikuambie kitu si mwisho wa ndoa yako, wanawake si warahisi kutoka kwenye ndoa namna hiyo na niwavumilivu mpaka basi. Acha kupaniki, acha kujidharau, mke wako hakudharau na kama ukiwa muwazi yupo tayari kukusaidia na kama ukijiamini hata unaweza kufurahia tendo la ndoa na ...

Usijilaumu kama mtu kakuacha baaada ya Kumgundua kwani angekuacha tu kwa sababu yoyote ile.

Image
  Unakuatana na mtu mnapendana sana, unamuamini anakujali na mnapanga mambo mengi sana, mnatumia muda mwingi pamoja na unaona kabisa kuwa huyu ndiyo mtu sahihi kwangu, anafaa kuwa mke au mume wangu. Lakini katika kipindi cha muda mfupi kunapita upepo flani, wakati wewe ulishajiweka kwake na kufunga milango mingine unakutana na kitu kidogo tu ambacho kinabadilisha kila kitu ulichokuwa unakiamini kuhusu huyo mtu. Unakutana na meseji moja tu ambayo labda alikosea na kumtumia mtu mwingine au alisahau kuifuta na kuiona kwako kunakufanya kujua kuwa kumbe kila kitu ulichokuwa ukikiamini kuhusu muhusika ni cha uongo. Unajaribu kuongea naye ili angalau kutaka kujua tatizo ni nini, kujua ulikosea wapi labda ukamfanya kuchepuka, ulifanya nini mpaka kufikia hatua ya yeye kukusaliti na kuwa na maisha mengine kabisa. Lakini pamoja na kwamba kosa ni lake basi anachukulia fursa hiyo ya wewe kujua madhambi yake kubadilika, anaacha kupokea simu zako, anaacha kukujali tena, hajali hisia zako, haombi ...

Je, wewe ni mtu wa kuachwa achwa? Wanaume hawatongozi kuoa wanatongoza Mahusiano

Image
Lengo la kwanza la mwanaume yeyote anapokutongoza kwa mara ya kwanza ni kutaka kufanya mapenzi na wewe. Hilo ndiyo lengo lake la kwanza, mengine huja huko baadaye mbele ya safari. Asilimia tisini ya anachokuambia mwanaume kabla ya kutembea na wewe ni uongo, ndiyo ni uongo na mara nyingi husema ili tu kukushawishi basi. Sasa dada zangu acheni kudanganyika na wale watu ambao anakuambia anataka kukuoa, hamna wiki kwenye mahusiano kashatangaza ndoa. Kila mwanaume ana rafiki yake mmoja, Dada yake, shangazi au Mama yake mdogo ambaye ni kwaajili ya kutambulishia michepuko yake mipya. Kwamba ili umuamini anakupeleka kabisa kwa Dada yake, sijui shangazi yake au Mama yake mdogo, wengine hata Mama zao wazazi. Utasikia binti anasema “Mama yake mdogo, shangazi yake, sijui dada yake ananipenda…” Acha kudanganyika huyo ni kazi yake, yaani mpo kama kumi ambao mnapendwa na huyo huyo. Sasa unaweza kuuliza kama ni hivyo nifanyeje? Unachotakiwa kufanya ni kuwa, ukitongozwa kubali kwakuwa na wewe unataka, ...