Posts

Showing posts from July, 2021

DALILI 7 ZA MWANAUME ALIEMCHOKA MPENZI WAKE.

Image
Wanawake ni itapendeza kama utaizingatia hii,ila kama haitakuwa na maana yote pia ni sawa pia. Kwa kawaida jambo lolote lina kuwa na ishara Fulani kabla ya kutokea tukio husika,pia hata hivo hivo katika mapenzi,kuna dalili zake pia,nimekuandalia dalili chache za mwanaume ambaye ameanza kumchoka mpenzi wake. Zama nami....... Dalili ya 1 Mwanaume anaanza kuonyesha hasira na kuhamaki kwa kila unachokifanya hata kama ni kitu kidogo. Hii ni kwasababu penzi limempungua au kumuisha na hivyo anakosa uvumilivu kwako. Anaweza kukupayukia hata ukiwa katikati ya watu, hatojali unavyojisikia kwa yeye kufanya hivyo. Utashangaa na kujiuliza mbona mwanzoni aliweza kunivumilia? Jibu ni kwamba penzi limepoa au kuisha Dalili ya 2 Kwa kawaida mwanaume anavyompenda mwanamke huwa na kiu ya kumfurahisha, hufanya vitu kuhakikisha mpenzi wake anatabasamu na anajisikia murua. Kila siku kiu ya mwanaume ni kuona mwanamke anatamani kuendelea kuwa ndani ya penzi hilo. Mapenzi yakiisha vitu hivi vyote vinapeperukia ...

DHANA YA UHABA WA WANAUME HUWAWEKA BAADHI YA WANAWAKE KATKA MAHUSIANO MAGUMU.

Image
Kuna wakati hutokea wanawake wakateswa sana kwenye uhusiano wao wa kindoa au kimapenzi na bado wakaendelea kukaa tu kwenye uhusiano huo. Inafikia hadi mtu anakufa huku akiona kabisa. Watu wengine huiita hali hii kuwa ni ujinga na wengine huita kulogwa au huelezea hali hii kwa njia ambayo haiwapi haki wanawake hao. Zipo sababu nyingi ambazo zinawafanya wanawake kuendelea kukaa kwenye mahusiano magumu au ndoa ngumu, bila hata kufikiria kuondoka. Sababu nyingine zinaweza kuonekana kama kituko, lakini ndizo zinazowafanya wang’ang’anie uhusiano huo au wafie kwenye uhusiano au ndoa hiyo. Kuna dhana imejengeke kwa baadhi ya wanawake kwamba wanaume ni wachache au hakuna wanaume wa kuoa. Dhana hii ambayo haina ukweli wowote, imewafanya baadhi ya wanawake kuishi katika mahusiano magumu na wenzi wao wakihofia kutoka au kuachana nao kwa sababu hawatapata mwanaume mwingine. Kuna wanawake wengi sana ambao wanagombea kupendwa, au wanajipendekeza ili wapendwe. Hawa ni wanawake ambao wana kasoro kubwa...

(BINTI YANGU YAJUE HAYA) NDOA INAANZA BAADA YA HARUSI.

Image
Mwanangu nisikufiche, watu wengi huchangia sherehe ili waje kula na kunywa na kuoneshana fahari, ukoo wa Mume na ukoo wa mke nao wanaoneshana umwamba hawa kwenye Send-off na hawa wanajibu kwenye harusi. Na ule usiku baada ya reception sijui ndio mnaita hivyo mnaingia kwenye gari kuelekea kwenye fungate(honey moon). Hapo hata wanakamati huwa wanakimbiana ninyi mkishaondoka kwani shughuli yao imeishia pale. Hata wasimamizi watawasindikiza mpaka chumba mnacholala kisha wanawaacha hapo. Lakini kazi yako ndio inaanzia hapo. Wewe humalizii siku ya harusi. Hapa ndio unaosha make up na kubandua hizo kope artificial na kucha na kuingia kwenye mapambano kupigania Ndoa yako. Ukweli ni kwamba wanaotarajia NDOA itakushinda ni wengi nikiwemo Mimi, na tunapokupigia simu kuuliza "Mnaendeleaje? " huwa tunatarajia jibu lolote kutoka kwako. Kwa sababu NDOA Inaanza baada ya harusi. Usiingie huko ndani kwenda kucheza. Naomba nikwambie kauli ngumu na ndio ukweli kwa sababu nakupenda. Hicho cheti ...

UMEKUBALI KUOLEWA KUBALI BASI KUACHANA NA NDUGU ZAKO, HUJAWACHOKA TU!

Image
Utakuta mwanamke analilia kuolewa, anahangaika sana kuomba na kusali, kutegeshea Mimba na hata kutafuta Mganga ili tu aolewe.anabahatika kweli anaolewa, anakutana na mwanaume anampenda na yuko tayari kutengeneza maisha. Lakini sasa binti anakua kama amesahau kitu huko kwao, kwanza kila siku anapiga simu kwao. Hii si mbaya kuwajulia hali, lakini itoshe tu uwajulie hali sio kila siku kumpa taarifa mume wako, mara Mama anakusalimia, Mama kasema hivi, Mama sijui vile, nilikua naongea na mdogo wangu, sijui kaenda shule, sijui nani kafanya hivi! Daaa mpaka inaboa, unaweza kuona kama kitu cha kwaida na inawezekana mume wako akakusikiliza kwakua anakupenda. Lakini Dada yangu nikuambie tu unaboa, hakuna mwanaume ambaye anataka kusikia stori za kwenu kila siku, hata kama si matatizo, hata kama ni furaha lakini kama kila siku ukiongea na ndugu yako unamuambia mume wako basi jua kuwa kashachoka kusikia. Tena haiishii hapo, mwanaume ambaye anasikia hivyo kila siku anakua na wasiwasi. Kwanza anawaz...

HII NI KWA WANAWAKE WOTE, HEBU SOMENI HAPA

Image
DEAR LADIES Ni jukumu lako kuwa romantic kwa mumeo. Aibu yako isikuzuie kuonyesha mapenzi yako kwa mume wako. Mtumie meseji mume wako anapokuwa kazini, muda mwingine hata kama yupo nyumbani mnaangalia TV chati nae katika mitandao ya kijamii (watsapp, Facebook etc) hata kama yupo mbele yako. Hii huleta faraja na ni njia mojawapo ya kuwa romantic kwa mwanaume wako. Jadiliana nae jinsi gani anavyokuvutia. Mnunulie zawadi hata leso, boxer, tai, viatu nk. Mnapokua mezani mkila pamoja labda nyama, mpe nyama kubwa kuliko zote. Kama muda unao mtengenezee keki na juice ya matunda na msuprise nayo. Wadada, tumieni sauti yenu laini kumbembeleza na kumdekea, muimbie mnapokua pamoja chumbani, acheni userious kama mpo kwenye kikao cha bodi ya Korosho. Mume wako anaporudi toka kazini usimkaribishe huku umenuna utafikiri shabiki wa Arsenal aliekosa kombe baada ya msimu wa ligi kuisha. Usimkaribishe mume wako huku mwili wako ukinukia mchuzi wa samaki au pilipili hoho, kuwa msafi na unukie. Wanaume hawa...

PUNGUZA KULALAMIKA KABLA HAJAACHA KUKUPIGIA SIMU KABISA!

Image
Nijambo la kawaida kumsikia mtu akilalamika kuwa mpenzi wangu, mume au hata mke wangu huwa hanipigii simu wala kunitumia meseji mara kwa mara, kila wakati nilazima nimuanze mimi, mtu analalamika na kujuiona kama vile hapendwi. Mara nyingi hii hutokea kwa wanawake na inauma sana kama kila siku wewe unakua mtu wa kumtafuta mpenzi wako, anakua hajali na unajiona kama unajipendekeza. Ulishawahi kuhisi hivyo, sasa wakati mwingine kweli inawezekana hakupendi, anakuchukulia poa kwakua anaona unampenda zaidi. Lakini wakati mwingine sio hivyo, mara nyingi na kwa idadi kubwa ya watu ambao huniomba ushauri kuhusu suala hili tatizo ni kwao hao wanaopiga simu mara kwa mara. Kwamba wewe ambaye unajiona kama unapenda zaidi kuliko mwenza wako ndiyo mwenye tatizo na si huyo unayeona hakujali. Tatizo kubwa nikuwa humpi muda mpenzi wako wa kukumiss mpaka kukupigia simu. Labda nifafanue kidogo katika maisha ya kawaida watu hupigiana simu wakiwa na shida flani, hasa wanaume, mpaka kuwe na kitu falani ndiyo...

ISHARA 13 ZA MWANAMKE MWENYE SIFA ZA MKE BORA (WIFE MATERIAL)

Image
Itatimia wakati flani ambapo utahitajika kuoa. Na kuoa huwa kuna harakati zake. Mtu hafai kuingia katika mpango wa ndoa bila ya kutambua yule ambaye ataona naye. Ikija katika maswala ya kuoa, utaskia wengi wakitumia maneno kama `wife material` ama `mke bora`. So utamtambuaje mwanamke ambaye ni wife material/mke bora? Kuna baadhi ya vigezo ambavyo watu huangalia na kutambua kama mwanamke ni wife material au la. Na muhimu zaidi huangalia tabia na matendo ya mtu. Kosa ambalo wengi hufanya ni kuwa wanakimbilia kuoa mwanamke bila ya hata kusoma tabia za wanawake hao ndio unapata wakati mwingine ndoa za baadhi ya watu zinakuwa na shida miaka michache baada ya kuoana. Katika somo la leo hapa tumekuja na tabia ambazo zitamtambua mwanamke ambaye ni wife material kwa urahisi sana. Twende kazi... Tabia za mwanamke ambaye ni wa kuoa (wife material) 1. Anakusikiliza wakati unaongea. Ijapokuwa hili linaonekana swala dogo, ikija kwa kuchagua mwanamke lina umuhimu mkubwa. Mwanamke ambaye anakusikiliza...