UKIONA MWANAMKE WAKO AMEACHA KULALAMIKA KUHUSU MAMBO ULIYOKUWA UNAMFANYIA JUA KUNA MAKUBWA YANAFUATA
:
1) Jambo la kwanza inawezekana kuwa kashaanza kukuchoka na hajali tena.
3) Jambo la tatu ni kwamba huyo mwanamke kashakukatia tamaa kuwa hutabadilika na kaamua kujipa furaha yake mwenyewe.
4) Jambo la nne wengi wakiona wanawake zao wapo busy na mambo yao udhani wana mwanaume mwingine sio kweli, mwanamke akichukia anachukia kweli kweli. Unakuta wala hachepuki, na wala hana mpango wa kukuacha, wala hana mpango wa kutafuta mtu mwingine.
5) Jambo la tano husiombe mkeo au mpenzi akae ajiulize mambo aya:
1} Hivi nahangaika nini?
2} Nitapiga kelele mpaka lini?
3} Nitajibiwa matusi mpaka lini?
4} Nitahangaika na wanawake zake katika mitandao mpaka lini?
5} Hivi mimi ni mtu gani kila siku kupekua simu yake na kukuta mapicha ya uchi?
6} Hivi huyu mwanaume ni pumzi kwamba nisipohangaika naye nitakufa?
Ayo ni maswali mabaya sana mwanamke akijiuliza, sasa ole wako apate jibu.
USHAURI WANGU:
Siku akijiuliza yale maswali 6, Mimi nitamsaidia kumpa jibu, hapo ndio utajua kuwa jela ya mapenzi ni mbaya kuliko ata keko na segerea.

Comments
Post a Comment